Designer Hebron Malele More information *Phone number 0659-994437*: hebronjohana@yahoo.com!!  NICE FOR ALL :

Thursday, 18 June 2015

Makala yetu ya HATUJACHOKA KUDANGANYWA. inaendelea fatilia.




1.    Ujinga, bila shaka hii ndio furaha ya watu hawa watangazania wasio na kumbukumbu, hayati baba wa taifa alipata kusema tunasumbuliwa na maladhi matatu na moja ya maladhi yale kama ninakumbukumbu ya kuniwezesha kuwa mkweli ni ujinga ambao mpaka baba wa taifa anapumzika kwa amani alionekana kwa dhati ya moyo wake akipigania janga la ujinga kwa kuwa katika kipindi chake tuliona na tumehadithiwa namna watu wa nyakati zake walivyopata elimu kwa raha mpaka kuweza kuwa wanakula mayai na karanga mashuleni na wengi wao wakisomeshwa bure ili kuja kulisaidia taifa la tanzania baadae wengine walipelekwa Cuba,Urusi na nchi mbalimbali ughaibuni ili kuweza kufuta ujinga na kuja kuwakomboa watanzania wakuzamia wakaishia huko,waliorudi na kutunufaisha tumewaona na wale wenye uelewa kuliko wengine baada ya kufutwa ujinga wakaona ni bora kutupandikiza ujinga kwa kuweka mifumo mibovu ya elimu mpaka elimu kuwa biashara,elimu sasa ni gharama kuliko hata ujinga wenyewe na hata elimu utayoipata baada ya kuinunua kwa gharama ya juu imekuwa haina msaada kutokana na ukosefu wa ajira,ugumu wa upatikanaji wa mitaji kwa ajili ya kukiajiri,na hata silabasi isiyomjenga mwanafunzi kujitegemea zaidi ya dhana ya ajira na kuwa na taifa lililokosa maadili kwa wale waliobahatika kushikwa mikono na kupata ajira katika ofisi za serikali. Asilimia kubwa ya watanzania ambao ni fungu la kukosa kwa maana kama umebahatika kupata kimoja hiki kingine sahau nikiwa na maana umebahatika kununua elimu sahau ajira.
2.    ukosefu wa elimu, linapokuwa linajadiliwa swala hili huwa napata shida kuelewa kuwa ndani ya bunge letu la jamhuri ya muungano wa Tanzania huwa linabaadhi ya wabunge kutoka mataifa mengine au wote ni watanzania kama jina la bunge letu linavyoitwa, wengi mtajiuliza kwa nini nimechelea kusema hivyo, ati watanzania kusoma bure haiwezekani kuanzia chekechea/vidudu mpaka elimu ya juu eti kwa kuwa serikali haina fedha za kutosha kuendesha zoezi hilo, lakini tujiulize ni kiasi gani kinatakiwa kila mwaka kwa ajili ya wanafunzi wenye vigezo vya kusoma mpaka ukomo wao kulingana na katiba ya Tanzania ya mwaka 1977, ambayo kwa kumbukumbu ndogo niliyonayo inasema yampasa mtu yeyote mwenye vigezo vya kusoma aweze kusoma ama kusomeshwa na serikali na kama atafikia vigezo vya kuajiriwa pia serikali imfanyie hivyo,sasa wale baadhi ya wabunge na mawaziri walioacha kuitwa wabunge ambao nina wasiwasi na uraia wao wanaposema serikali haina uwezo wa kusomesha na kutengeneza ajira wakati huo huo tukirejea kwenye masakata ya ESCROW,KIGODA,MEREMETA,IPTL,RICHMOND,NBC,MISHAHARA HEWA,BUNGE LA KATIBA LILILOBADILISHA MAUDHUI YA RASIMU YA KATIBA,MIKATABA INAYOSAINIWA MAHOTELINI,KUSAMEHE KODI,UTAIFISHAJI WA VIWANDA NA MASHIRIKA YA UMMA PAMOJA NA KUYAFILISI KUTOKANA NA UTENDAJI MBOVU MFANO RELI YA KATI,TTCL,AIR TANZANIA,URAFIKI,SUNGURA N.K usishangae kwanini nimeandika kwa herufi kubwa labda herufi ndogo zisingeonekana vizuri, lakini haya yote ndugu yangu kwao yamewezekana na yanendelea kuwezekana kwao ila sio kumpeleka mtoto wako shule akapate elimu ya bure au kufuta ujinga kama walivyofanyiwa wao hawa ambao wengi wao nimeanza kuutilia shaka uraia wao.
3.    Ukosefu wa matibabu thabiti, hapa unaweza kuandika makala huku unatokwa na machozi ndugu msomaji yaani hata takwimu kuzifuatilia naogopa kwa sababu haziendani na miaka hamsini ya uhuru wa nchi yetu. Wahanga wakuu hapa ni wakina mama,wakina mama wajawazito na watoto. Siku hizi ukienda hospitali hasa hizi hospitali zetu za umma/serikali utaambulia ushauri na si matibabu, kwasababu unaenda hospitali ukiwa mgonjwa mahututi kama hauna fedha basi imekula kwako utamwona daktari atakushauri na kukueleza dalili za ugonjwa ulionao ni ugonjwa gani alafu kauli ya mwisho itakuwa dawa zinapatikana katika duka fulani mtaa fulani hapa zimetuishia na wala si kosa la daktari kwani ukienda kwa Msd (medical store department utaambiwa ni jumla ya kiasi gani wanaidai serikali) kwa kweli inasiitisha ikiwa wakati huo huo kuna baadhi ya watanzania wenzetu wanakatwa fedha kwa minajiri ya kuwa na bima za afya zao lakini wanavyokutana navyo hospitali si vya kusimulia.vijijini kilio hiki ni kikubwa zaidi kwani hupelekea watu hata kufa/kujifungulia njiani kutokana na kukosa hospitali au zahanati karibu na makazi sawa Tanzania ni nchi ya Amani na Upendo je upo wapi Upendo na Amani kwa watoto vichanga na mama zao wanao fariki njiani kabla ya kufika hospitali ama zahanati???! Jamani watangaza nia tuwe na huruma mliyotufanyia yanatosha na sasa ni wakati wa kuwapa wengine vijiti mtatumaliza sasa sijui mtatawala viumbe gani kama watanzania wanaisha kwa Malaria,kifua kikuu,ukimwi,kipindupindu,saratani,kisukari,presha na hasa kuwapoteza malaika ambao ni kizazi cha kesho wakati wa kujifungua.
4.    Ukosefu miundombinu imara na thabiti,hapa ndipo serikali inapoanzia kuwa serikali ya historia tumejenga barabara kilimita 1000,mara kilomita 7000 sawa tumekubali je baada ya kujenga kilimita zote hizo mbona foleni kwenyi miji hazipungui,mazao kutoka mashambani yameendelea kuwa juu kutokana na gharama za usafirishaji,watanzania wamekua wakipungua kila siku kutokana na ajali za mabarabarani ukiuliza sababu dereva alikuwa akikwepa shimo la barabara iliyopitishwa bajeti yake mwaka juzi wakati wenzetu wana barabara zina umri wa uhuru wetu na hazina mashimo haya yote watangaza nia ni mazao ya chama chenu na uongozi wenu sasa napata wakati mgumu mnaposema nyinyi wenyewe mtafanya tofauti na mlivyokuwa mkifanya awali. Kwa lugha nyepesi kauli na hotuba zenu ni nzuri hasa mngekuwa mnatokea upande wa pili wa shilingi,ila kwa staili hii ya kuvaa ngozi ya kondoo ndani chui kwa kweli kauli zenu hazina mashiko katika serikali ya kichwa changu mpaka pale hata mmoja wenu akaweza kunieleza vizuri nimuelewe alikuwa wapi wakati wenzake wakifanya kazi kwa umoja kutufikisha hapa tulipo maana kidole kimoja hakivunji chawa.
5.    kuongezeka kwa gharama za maisha wakati kipato ni kidogo
6.    ongezeko kubwa la aliyenacho na asiyekuwa nacho
7.     ufisadi/matumizi mabaya ya madaraka, nukuu” waziri wa kilimo na ushirika,Wasira  amesema ndani ya ccm hakuna mafisadi bali neno fisadi ni msamiati unaotumiwa na wapinzani kama njia ya kuwakashifu makada wa chama tawala. Wasira alitoa kauli hiyo wakati alipotakiwa na waandishi wa habari kueleza namna atakavyopambana na mafisadi ikiwa atapata fursa ya kuliongoza Taifa. Wasira alibainisha kuwa katika mijadala mbalimbali swali la ufisadi halipaswi kulizungumza kwa kuwalenga watu na badala yake linapaswa kujadiliwa kama hoja na kutafutiwa ufumbuzi kama ilivyo swala la umaskini na uwajibikaji. “ninavyofahamu mimi ndani ya ccm hakuna mafisadi,lakini kama hoja ufisadi sitaifumbia macho,nitazungumza na kuishughulikia”, alisema Wasira. Kweli ama si kweli kwa lugha nyingine ni uongo ama si uongo ninatumaini jibu unalo wewe mtanzania katika serikali ya kichwa chako kazi kumkichwa
8.    ukosefu wa ajira kwa vijana na mifumo ya uwekezaji mzuri wa akiba uzeeni kwa wariojiajiri na kukosa ajira.
Na kuondoa dhana ya demokrasia ya utawala wa watu kwa ajili ya watu na unao tawaliwa na watu kwa sababu binadanu wa kawaida ukimpatia majanga kumi kama tulivyoyaorodhesha hawezi kuishi kama binadamu ni lazima atakengeuka na kuwa kiumbe wa aina nyingine ali aweze kupata maslahi yake kama binadamu na hapa ndipo tunawapata wadai haki na wanaobatizwa majina ya waasi.
Makala hii imeandaliwa na
Godlove Malele
p.o.box 7583
Dsm
godlovemalele@yahoo.com

No comments:

Post a Comment