Designer Hebron Malele More information *Phone number 0659-994437*: hebronjohana@yahoo.com!!  NICE FOR ALL :

Monday, 15 June 2015

YALIYOJILI:JUU YA USAJILI ULAYA.





Chelsea wamemsajili Radamel Falcao, 29 kutoka Monaco, na wanatarajia kutangaza mkataba wake wiki ijayo (Daily Star), mshambuliaji wa Manchester United Robin van Persie anasisitiza kuwa anataka kubakia Old Trafford licha ya taarifa kuwa huenda akaondoka (Daily Mirror), Manchester City ambao wamehusishwa na Raheem Sterling, Paul Pogba na Kevin De Bruyne wataendelea na usajili licha ya wasiwasi wa kuchukuliwa hatua na Uefa kuhusiana na sheria za kifedha za uhamisho (Manchester Evening News) Manchester United wanapanga kutoa pauni milioni 30 kumchukua kiungo mshambuliaji Filipe Anderson, 22 kutoka Lazio (Sun), Man Utd pia inaweza kumsajili kipa wa Ajax Jasper Cillissen, 26, kuziba pengo la David De Gea, 24, ambaye anahusishwa kwenda Real Madrid (Daily Telegraph), mashambuliaji wa Sevilla, Carlos Bacca, 28, ambaye anaripotiwa kutakiwa na Man Utd na Arsenal, anataka kwenda Roma ya Italia (Daily Mail), West Ham wanatka kumsajili mshambuliaji wa QPR Charlie Austin, 25. Mchezaji huyo anawindwa na Southampton na Newcastle United (London Evening Standard), Everton wanafikiria kumchukua mshambuliaji wa Arsenal Lucas Podolski , 29 ambaye amecheza kwa mkopo Inter Milan msimu uliopita (Daily Star), mshambuliaji kutoka Croatia anayechezea Atletico Madrid Mario Mandzukic, 29, huenda akachukuliwa na Wolfsburg, iwapo Bas Dost, 26 ataondoka Ujerumani na kwenda Newcastle. Mandzukic pia ananyatiwa na Liverpool na Manchester United (AS), kiungo wa Arsenal Mesut Ozil amesema wachezaji wenzake wa Ujerumani Mats Hummels na Benedikt Howedes wana viwango vya kuwika Uingereza. Hummels, 26, amehusishwa na kuhamia Man Utd, huku taarifa zikidai kuwa Howedes, 27, ananyatiwa na Arsenal (Guardian) meneja wa Chelsea Jose Mourinho anakaribia kusaini mkataba mpya wa miaka minne wenye thamani ya pauni milioni 30 kwa mwaka kusalia Stamford Bridge (Daily Mail). Uhamisho uliothibitishwa nitakujulisha ukithibitishwa. Tetesi nyinine kesho tukijaaliwa.

No comments:

Post a Comment