Designer Hebron Malele More information *Phone number 0659-994437*: hebronjohana@yahoo.com!!  NICE FOR ALL :

Wednesday, 17 June 2015

#MAKALA YA LEO:WATANZANIA WENYE NIA PANA NJIA, NI KWELI HATUJACHOKA KUDANGANYWA.



Makala
Hakuna mtu aliye na kumbukumbu za kutosha kumwezesha kuwa muongo”
 Abraham lincoln (1809-1865)
Baada ya kumsoma mwanafalsafa huyu na falsafa zake mbalimbali kwa leo nimetokea kuvutiwa na falsafa hii hasa kutokana na kipindi kigumu tulichopo kwa wakati huu wa kuelekea uchaguzi mkuu ambapo kila mwanasiasa anataka kuwafanya watanzania ni kichwa cha mwendawazimu kama ambavyo alipata kuzungumza miaka fulani mzee wa ruksa na raisi mstaafu wa awamu ya ya pili Ndugu, Ali Hassan Mwinyi.
Ni kwaninini natokea kuvutiwa na mwanafalsafa huyu wa kutokea ughaibuni aliyepata kuishi mwanzoni mwa miaka ya 1800, hili naweza kuliweka wazi ni kwakuwa viongozi wetu wengi wa sasa ambao wanajibatiza au tumewabatiza majina mapya ya watangaza nia ya kuwania uraisi kupitia chama cha mapinduzi ccm wanasadifu kwa hali ya juu kabisa kauli hii iliyowahi kuzungumzwa na mwanafalsafa aliyewahi kuwa raisi wa taifa kubwa la marekani akikumbukwa kuwa mmoja ya mwasisi mkubwa wa demokrasiahasa baada yakutoa ile  kauli maarufu ya “democracy is the government of the people for the people by the people”  kwa lugha yetu hadhimu ya kiswahili angelisema” demokrasia ni utawala wa watu kwa ajili ya watu unao tawaliwa na watu”
Tukirejea muongozo wa makala yetu,” hakuna mtu aliye na kumbukumbu za kutosha kumwezesha kuwa muongo” nashawishika kabisa kusema uongo ni dhambi tena kuifanya kwa makusudi na kuirudia rudia inaweza ikawa ni dhambi isiyosamehewa kabisa na wananchi ambao ndio wahanga wakuu wa maisha magumu yanayoambatana na
1.    njaa,
2.    Umaskini, nukuu kutoka kwa mmoja ya watangaza nia “nachukia sana umaskini”,na kuuchukia kwake umaskini ndio kumemfanya awaze kutangaza nia ya kugombea uraisi na mtu huyu amekuwako serikali tena katika nyadhifa za juu kabisa kwa zaidi ya awamu nne{4} za miaka mitano mitano akiwa anaingia kwenye baadhi ya vikao vya baraza la mawaziri na akiwa ameshawahi kuwa mmoja ya watu wa juu kabisa katika ngazi ya chama kwa ajili ya kutengeneza sera za chama chake na kuwa kampeni meneja wa raisi anayeenda kumaliza majukumu yake hivi karibuni tena akisimama na kujinadi mbele ya wananchi jinsi alivyoweza kuyatimiza baadhi ya majukumu yake hayo katika kipindi kilichopita…hapo ndipo ninapo jiuliza kutokana na jinsi anavyouchukia umaskini mpaka kumpelekea kuwa mmoja ya watangazania ni kwanini asingeweza kutumia nguvu na ushawishi wake wa mafuriko yasisyoweza kuzuiliwa kwa mkono kuweza kupiga vita umaskini kwa kipindi chote alichokuwa akihodhi madaraka na nafasi za juu ndani ya chama chake na serikali Ama kweli Abraham Lincoln have never died he just passed away (kwa lugha yangu tamu na nzuri ya kiswahili ni kwamba Abraham Lincoln hakufa bali amepita kama njia hii ni kutokana na kwamba maneno mengi yaliyowahi kuzungumzwa na watu wa kariba yake yameendelea kuishi, hakuna mtu aliye na kumbukumbu za kutosha kumwezesha kuwa muongo. Miaka ishirini{20} ni sawa na awamu nne{4} za miaka mitano mitano{5},pia ni sawa na miaka ishirini ya kijana mpiga kura halali wa kitanzania ambae alizaliwa wakati watangaza nia wengi wakianza kuitumikia serikali katika nyadhifa za uwaziri,ubunge na nafasi mbalimbali ndani ya chama chao,na wameendelea kuwa huko mpaka sasa je ni kweli watu hawa wanauchukia umaskini kiasi cha kuwashawishi vijana hawa waliokulia katika majanga kumi tuliyoyataja hapo juu wanaweza kuwashawishi vijana hawa ambao ni 60% ya idadi ya watanzania,kwa kweli mjifunze kusoma alama za nyakati nafikiri vijana wezangu,wakina mama na wazee tunahitaji mabadiliko ya kweli.
     Makala hii inaendele siku nyingine endelea kufatilia page hii ya *SAHARA SUPER GYM*
                                          
Makala hii imeandaliwa na
Godlove Malele
p.o.box 7583
Dsm
godlovemalele@yahoo.com

No comments:

Post a Comment