Designer Hebron Malele More information *Phone number 0659-994437*: hebronjohana@yahoo.com!!  NICE FOR ALL :

Thursday, 11 June 2015

YALIYOJILI:Iker Casillas amekubali kuondoka Real Madrid.




Iker Casillas amekubali kuondoka Real Madrid na nafasi yake itachukuliwa na David De Gea, kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na shirika la habari la taifa la Spain- Television Espanola. Nahodha huyo wa Real Madrid bado ana miaka miwili katika mkataba wake Santiago Bernabeu, na kwa mujibu wa taarifa hizo, aliambiwa na Real Madrid kuhusu nia ya kusajili kipa mwingine msimu huu. Madrid wanatarajiwa kwa kiasi kikubwa kukamilisha uhamisho wa David De Gea kutoka Manchester United. Wakati Casillas, 34, akisema mara kwa mara kuwa angependa kumaliza mkataba wake, lakini pia yuko tayari kuondoka. Television Espanola imesema karibu vilabu kumi vimeonesha nia ya kumsajili Casillas.
 

No comments:

Post a Comment