Designer Hebron Malele More information *Phone number 0659-994437*: hebronjohana@yahoo.com!!  NICE FOR ALL :

Thursday, 11 June 2015

YALIYOJILI:TETESI ZA SOKA ULAYA.




Meneja wa Manchester City Manuel Pellegrini ameahidiwa kupewa fedha za kupindukia ili kuibadili kabisa timu hiyo iweze kutawala Ulaya (Sun), Pellegrini anataka kumsajili kiungo wa Juventus kutoka Ufaransa, Paul Pogba, 22, na pia mshambuliaji wa Liverpool Raheem Sterling, 20 (Daily Mail), mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzima, 27, huenda akajiunga na Manchester United katika uhamisho utakaoshuhudia kipa David De Gea kuondoka Old Trafford kwenda Bernabeu (Telegraph), Arsenal watajaribu kumnunua kipa Iker Casillas, 34, iwapo Real watakamilisha usajili wa David De Gea (London Evening Standard), Abou Diaby, 29, huenda akapewa nafasi ya kuendelea kusalia Arsenal kwa mkataba wa 'kulipwa-kwa-kucheza' licha ya kutajwa katika orodha ya wachezaji walioachwa (Times), kiungo wa zamani wa Chelsea Kevin De Bryne, 23, huenda akarejea England baada ya mchezaji huyo wa kimataifa wa Ubelgiji kuthibitisha kuwa wakala wake amekuwa na mazungumzo na Manchester City (Sky Sports), meneja wa Chelsea Jose Mourinho amepigwa marufuku kuendesha gari kwa miezi sita baada ya kukamatwa akiendesha gari kwa kasi ya maili 60 kwa saa kwenye eneo la maili 50 kwa saa (Mirror), Chelsea wamejaribu kuwakatisha tamaa wanaomtaka kipa Thibault Courtois, 23, kwa kumuwekea bei ya pauni milioni 73 (Telegraph), beki wa kulia wa England Glen Johnson, 30, anatarajiwa kujiunga na Besitkas ya Uturuki baada ya kuruhusiwa kuondoka na Liverpool (Liverpool Echo), Manchester City watamruhusu Micah Richards, 26, kuondoka lakini watabaki na kipa Richard Wright, 37 ambaye hajacheza mechi hata moja tangu alipojiunga nao mwaka 2012 (Manchester Evening News), Tottenham wanataka kumsajili beki wa kulia wa Burnley Kieran Trippier ambaye amehusishwa na Liverpool na Southampton (Mirror), Inter Milan wanataka kumsajili Javier Hernandez ambaye amerejea Manchester United baada ya kucheza kwa mkopo Real Madrid msimu uliopita. United wanataka euro milioni 15 kwa Chicharito (Tuttosport), Real Madrid watatoa dau rasmi kumtaka David De Gea wiki hii, lakini Manchester United watataka kumchukua Karim Benzima kama sehemu ya uhamisho huo. Louis van Gaal pia anamtaka kipa wa Chelsea Petr Cech (Daily Telegraph), Barcelona hawataki tena kumsajili kiungo wa Borussia Dortmund Ilkay Gundogan kwa sababu anataka mshahara mkubwa wa euro milioni 10 kwa mwaka (Bild), Everton wanataka kumsajili mshambuliaji wa Marseille Dimitri Payet (The Guardian), Roma wameonesha dalili za kumtaka mshambuliaji wa Everton Romelu Lukaku (Daily Mail), Southampton wanapanga kutafuta kiungo wa kuchukua nafasi ya Morgan Schneiderlin anayedhaniwa kuelekea Old Trafford. Dau lao la pauni milioni 12 kumtaka kiungo Grzegorz Krychowiak limekataliwa (Daily Express). Uhamisho uliothibitishwa nitakujulisha ukithibitishwa. Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Cheers!

No comments:

Post a Comment