Designer Hebron Malele More information *Phone number 0659-994437*: hebronjohana@yahoo.com!!  NICE FOR ALL :

Sunday, 7 June 2015

YALIYOJILI:Watu wasiofahamika wamevamia ofisi mpya ya chama cha Demokrasia na maendeleo Chadema Tawi la Mburahati kwa madoto.




Watu wasiofahamika wamevamia ofisi mpya ya chama cha Demokrasia na maendeleo Chadema Tawi la Mburahati kwa madoto na kubomoa ofisi hiyo bila ya kutoa taarifa yoyote kwa uongozi wa ofisi hiyo.
ITV imefika eneo la Mburahati kwa madoto zilipo ofisi hizo za Chadema na kukuta upande wa mbele wa ofisi hiyon ukiwa  umebomolewa na baadhi ya vitu kuvunjwa  huku uongozi wa ofisi hiyo ya Chadema ukielekezea lawama kwa serikali ya mtaa wa Mburahati kwa madoto kwa kuhusika na ubomoaji huo pasipo kufuata taratibu za ubomoaji.

Akijibu tuhuma hizo afisa mtendaji wa kata hiyo ya Mburahati hiyo Bi.Scholastica Matinde amesema sheria hairuhusu kwa chama chochote cha siasa kuweka ofisi kwenye maeneo ya masoko kama ambayo chama hicho cha Chadema kilivyofanya.
 PICHA NYINGINE YA TUKIO 



No comments: